Tuesday, 25 January 2022

Makaburi yaliyo na 'ujumbe kutoka kuzimu' yagunduliwa Misri

Makaburi yaliyo na 'ujumbe kutoka kuzimu' yagunduliwa Misri

Makaburi ya zamani ambayo yana majeneza kadha yaliyotengenezwa kwa mawe, na mkufu ulio na "ujumbe kutoka kuzimuni" vimegunduliwa nchini Misri.
Ugunduzi huo umefanywa Minya, kusini mwa Cairo. Makaburi yaliyogunduliwa ni ya zaidi ya miaka 2,000 iliyopita na shughuli ya ufukuzi inatarajiwa kuchukua miaka takriban mitano.

Waziri wa mambo ya kale Misri Khaled al-Enany amesema makaburi hayo yana majeneza 40, vito, vyungu na barakoa ya dhahabu.
Amesema kuna mashimo ya kuwekwa majeneza chini ya ardhi ambayo ni ya enzi za Mafirauni hadi enzi za Wagiriki mnamo mwaka 300BC hivi.
"Huu ni mwanzo tu wa 7ugunduzi huu mpya," aliwaambia waandishi wa habari.
"Karibuni tutaanza kuongeza kivutio kingine cha mambo ya kale Misri."

No comments:

Post a Comment

type your message here

Top Post

BINAMU YAKE HALAND NI MOTO MWINGINE

Binamu yake Haland ni balaa lingine ambalo hukulijua. Unajua kafanya nini? Amecheza mechi 37... Ndani ya mechi 37 unajua kashind...