Makaburi yaliyo na 'ujumbe kutoka kuzimu' yagunduliwa Misri
Makaburi ya zamani ambayo yana majeneza kadha yaliyotengenezwa kwa mawe, na mkufu ulio na "ujumbe kutoka kuzimuni" vimegunduliwa nchini Misri.
Ugunduzi huo umefanywa Minya, kusini mwa Cairo. Makaburi yaliyogunduliwa ni ya zaidi ya miaka 2,000 iliyopita na shughuli ya ufukuzi inatarajiwa kuchukua miaka takriban mitano.
Waziri wa mambo ya kale Misri Khaled al-Enany amesema makaburi hayo yana majeneza 40, vito, vyungu na barakoa ya dhahabu.
Amesema kuna mashimo ya kuwekwa majeneza chini ya ardhi ambayo ni ya enzi za Mafirauni hadi enzi za Wagiriki mnamo mwaka 300BC hivi.
"Huu ni mwanzo tu wa 7ugunduzi huu mpya," aliwaambia waandishi wa habari.
"Karibuni tutaanza kuongeza kivutio kingine cha mambo ya kale Misri."
No comments:
Post a Comment
type your message here