Michezo(Sports)

Romario kuwania ugavana Rio de Janeiro, Brazil

 Seneta wa Brazil na mchezaji wa zamani Romario de Souza atawania wadhfa wa ugavana wa Rio de Janeiro mwezi Oktoba.

Jimbo hilo limekumbwa na ghasia na liko katika hatari ya kufilisika.

Mshindi huyo wa kombe la dunia la mwaka 1994 anajejulikana kama Romario anasema kuwa kampeni yake itaangazia kukabiliana na matatizo hayo.

Atakuwa mgombea wa chama cha mrengo wa kati cha Podemos. Amesifiwa kuwa seneta katika vita vyake dhidi ya ufisadi katika kandanda.

''Katika wakati huu wa ghasia, mabadiliko yanahitajika haraka. Rio ilikuwa na matatizo ya kiusalama, lakini sio kama sasa'' , mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 52 alisema siku ya Jumamosi akitangaza kuwania wadhfa huo.

Romario awali aliwania kuwa Meya wa Rio de Janeiro, lakini akajiondoa baadaye.Haki miliki ya picha

Romario awali aliwania kuwa Meya wa Rio de Janeiro, lakini akajiondoa baadaye
''Sina uzoefu wa kusimamia. Itakuwa kutokana na majaliwa ya Mungu , kwa mara ya kwanza kuonyesha kwamba nimekuwa na fursa kuonyesha kile nilichojifunza katika maisha yangu''.

Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona kwa sasa anachunguzwa kwa madai ya kuficha mali yake kwa lengo la kukwepa kulipa deni, kulingana na vyombo vya habari vya Brazil.
Amekana madai hayo.







Sudan: Faru wa kipekee aliyekuwa amesalia duniani afa

Sudan, faru pekee wa kiume aina ya Northern White Rhino (Faru Weupe wa Kaskazini) aliyekuwa amesalia hai duniani, amekufa akiwa na miaka 45, shirika la Ol Pejeta limetangaza.
Faru huyo alikuwa akitibiwa kwa muda na matabibu katika shamba kubwa la uhifadhi wa wanyama la kituo hicho kwa muda kutokana na matatizo yaliyotokana na kuzeeka kwake.
Alikuwa na vidonda ambavyo vilikuwa vinakosa kupona kutokana na umri wake.
Shirika la Ol Pejeta limesema hali yake ilidhoofika sana katika kipindi cha saa 24 zilizopita.
"Hakuweza hata kusimama na alikuwa anateseka sana," Ol Pejeta wamesema kupitia taarifa.
Ripoti: Faru John alikufa kwa kukosa uangalizi wa karibu
"Matabibu wa wanyama kutoka kituo cha uhifadhi wa wanyama cha Dvur Kralove kutoka Jamhuri ya Czech, Ol Pejeta na Shirika la Wanyamapori kenya waliamua kukatisha uhai wake."
Sudan alikuwa maarufu sana duniani na alikuwa nembo ya kutetea juhudi za kupigana na ujangili na kuwaokoa wanyama walio katika hatari ya kuangamia.

Alinusurika kuuawa porini alipohamishiwa katika kituo cha kuhifadhi wanyama cha Dvur Kralove nchini Jamhuri ya Czech miaka ya 1970.
Mwaka 2009, alirejeshwa Afrika na kuanza kutunzwa katika kituo cha Ol Pejeta katika jimbo la Laikipia.



No comments:

Post a Comment

type your message here

Top Post

BINAMU YAKE HALAND NI MOTO MWINGINE

Binamu yake Haland ni balaa lingine ambalo hukulijua. Unajua kafanya nini? Amecheza mechi 37... Ndani ya mechi 37 unajua kashind...